• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Historia ya Mkoa

Ndugu Msomaji Karibu katika tovuti rasmi ya Mkoa wa Singida. Mkoa wa Singida upo katikati ya Tanzania Bara. Mji wake Mkuu ni Singida na ni njia panda muhimu kwa usafiri wa barabara kwenda Kaskazini, Magharibi, Kusini na Mashariki.

Singida inapakana na Mkoa wa Manyara kwa upande wa Kaskazini, Mkoa wa Dodoma upande wa Mashariki, Mikoa ya Mbeya na Iringa upande wa Kusini na Mikoa ya Tabora na Simiyu upande wa Magharibi.

Mkoa wa Singida ulianzishwa rasmi tarehe 15 Oktoba, 1963 ambapo kabla ya hapo ulikuwa ni Wilaya ya Jimbo la Kati (Central Province) uliojumuisha Mkoa wa Dodoma.

Mkoa wa Singida uko katikati ya Tanzania, kati ya Longitudo 33027’5’’ na 35026’0’’ mashariki ya Greenwich, na kati ya latitudo 3052’ na 7034’ Kusini mwa Ikweta.

Mkoani Singida ndipo kuna eneo eneo rasmi ambalo lilibainishwa na vipimo vya kitaalamu vyenye namba 9305404.35, 698978.015 kuwa ni katikati mwa Tanzania bara yaani Central point of Tanganyika, ambapo ni katika kitongoji cha Darajani, Kijiji cha Chisingisa kilichopo kata ya Sasilo, tarafa ya Nkonk’o Wilaya ya Manyoni.

Mkoa wa Singida una Wilaya 5 ambazo ni  Singida, Iramba, Manyoni, Mkalama na Ikungi; zenye Halmashauri 7 za Singida, Singida Manispaa,  Iramba, Manyoni, Mkalama, Ikungi na Itigi. Aidha Mkoa una Tarafa 21, kata 136, Vijiji 442, vitongoji 2,309 na majimbo ya uchaguzi 8.

Ukubwa wa eneo la Mkoa wa Singida ni kilomita za mraba 49,341 sawa na asilimia 6 ya eneo la Tanzania Bara ambapo kati ya hizo kilomita za mraba 11,340 zinafaa kwa kilimo sawa na asilimia 23 ya eneo lote la Mkoa. 

Kwa upande wa hali ya hewa Mkoa wa Singida hupata mvua kwa kipindi kimoja cha mwaka (mwezi Novemba hadi Aprili) kwa wastani wa milimita 500 – 800 kwa mwaka na  wastani wa hali ya hewa ni nyuzi joto 15 – 30 kutegemea msimu na mwinuko wa ardhi. Kutokana na hali ya hewa, Mkoa wa Singida ni miongoni mwa Mikoa iliyopo kwenye ukanda wa unaopata mvua kidogo.

Kwa miaka ya karibuni wastani wa mvua umekuwa ukipungua kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoendelea kote Duniani.  Kwa mfano mwaka 2008/2009 kiasi cha mvua kilichorekodiwa katika kituo cha hali ya hewa Singida ni mm 778, mwaka 2009/2010 mm 641 na  mwaka 2010/2011 mm 425.7, mwaka 2011/2012 mm 582 na mwaka 2012/2013 mm 821.

Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa Mkoa wa Singida ni 1,370,637 ikiwa wanaume ni 677,995 na wanawake ni 692,642 huku kaya zikikadiriwa kuwa 225,670 ambapo kaya 189,115 zinajishughulisha na kilimo.

Shughuli za kiuchumi Mkoani Singida ni pamoja na kilimo ambacho huajiri wastani wa asilimia 86 ya wakazi wote. Mazao ya kipaumbele kwa upande wa chakula ni uwele, mtama, mihogo na viazi vitamu  na kwa upande wa mazao ya biashara ni alizeti, vitunguu, pamba na ufuta. Shughuli nyingine za uzalishaji mali ni ufugaji, uchimbaji mdogo wa madini, viwanda vidogo na biashara.

Pato la Mkoa ni Sh. 978,701,000 huku pato la mwananchi likiwa ni Sh. 697, 667 kwa mujibu wa taarifa za mwaka 2013.

Uongozi na Utawala wa Mkoa umekuwa ukibadilika mara kwa mara kulingana na mabadiliko ya Kitaifa. Tangu Mkoa uanzishwe hadi sasa Mkoa umeongozwa na jumla ya Wakuu wa Mikoa 18 kwa vipindi tofauti.    

Orodha ya Wakuu wa Mikoa waliofanya kazi Mkoani Singida tangu uanzishwe ni kama ifuatavyo:

1.     Bw. Dantes Ngua     1963 – 1964

2.     Bw. Peter Kisumo    1964 – 1965

3.     Bw. Rajabu Semvua 1965 – 1969

4.     Bw. Kapilima Kapilima    1969 – 1971

5.     Bw. Kingunge N. Mwiru   1971 – 1972

6.     Bw. Moses Nnauye   1972 – 1975

7.     Bw. Charles Kileo    1975 – 1977

8.     Brigedia Silas Mayunga   1977 – 1978

9.     Bw. Abdallah Nungu        1978 – 1981

10.   Capt. Peter N. Kafanabo   1981 – 1986

11.   Prof. John B. Machunda  1986 – 1987

12.   Maj. Gen. Mwita C. Marwa       1987 – 1990

13.   Bw. Gallus N. Abedi 1990 – 1993

14.   Bw. Abubakary Y. Mgumia       1993 – 1997

15.   Col. Anatoli N. A. Tarimo 1997 – 2002

16.   Bibi Halima Y. Kasungu   2002 – 2006

17.   Dr. Parseko V. Kone 2006 – 2016

18.   Mhandisi Mathew J. Mtigumwe Machi - Disemba 2016

19.  Dkt Rehema Nchimbi Disemba 2016 - Mei 2021.

20. Dkt Binilith Saatano Mahenge Mei 2021 hadi sasa

Kwa upande wa ngazi ya Mtendaji Mkuu wa Serikali katika Mkoa, Serikali ya Mkoa imekuwa inaongozwa na Wakurugenzi wa Maendeleo wa Mkoa tangu mwaka 1972 na baadaye mwaka 1997 chini ya Sheria Na. 19 ya Tawala za Mikoa – (Regional Administration Act Na. 19)  Makatibu Tawala wa Mikoa (Regional Adiministrative Secretaries – RAS) waliteuliwa kuongoza Sekretarieti za Mikoa ikiwa ni njia ya kuimarisha uwajibikaji na utoaji huduma bora kwa wananchi.

Wakurugenzi wa Maendeleo walioongoza Mkoa tangu 1972 ni kama ifuatavyo:-

1.     Bw. M. Jabiri Kigoda        1963 – 1964

2.     Bw. C. M. Joachim   1972 – 1974

3.     Bw. C. L. Kombo      1974 – 1975

4.     Bw. Crispin Duncan Mbapila   1976 – 1977

5.     Bw. I. Abubakar       1978 - 1983

6.     Bw. L. M. Rimisho   1984 – 1985

7.     Bw. A. S. Kaduri      1985 – 1988

8.     Bw. A. A. K. Mwasajone   1988 - 1989

9.     Bw. T. N. Machume 1989 – 1991

10.   Bw. Fredrick Nyelwa Kisenge   1991 – 1994

11.   Bw. Alfred Francis Fuko  1994 – 1995

12.   Bw. Emanuel Petro Mazalla     1995 – 1997

Makatibu Tawala wa Mkoa waliouongoza Mkoa tangu mwaka 1997 ni kama ifuatavyo:-

1.     Bw. Martin Odilo Mgongolwa   1997 – 2004

2.     Bw. Zawadiel Mchome     2004 – 2006

3.     Bibi Dyness G. Senyagwa 2006 – 2007

4.     Bw. Hussein A. Kattanga 2007 – 2009

5.     Bw. Godfrey S. Ngaleya    2009 – 2010

6.     Bw. Liana A. Hassan        2010 – 2015

7.    Bw. Festo L. Kang’ombe    2015- 2016

 8.    Dkt. Angelina M. Lutambi   May 2016 - Juni 2021.

9.  Bi. Dorothy Aidan Mwaluko Juni 2021 hadi sasa

ZIFUATAZO NI BAADHI YA PICHA ZA WAKUU WA MIKOA WALIOWAHI KUFANYA KAZI MKOANI SINGIDA;

Mhe. Dantes Ngua  - Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1963-1964 (wa kwanza kushoto)



Mhe. Peter Kisumo – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1964-1965 (aliyevaa kiraia)


Mhe. Rajabu Semvua – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1965 – 1969


Mhe. Kapilima Kapilima – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1969 – 1971

Mhe. Kingunge Ngombale Mwiru – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1971 – 1972.








Mhe. Moses Mnauye – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1972 – 1975 (aliyevaa miwani) 



Mhe. Charles Kileo – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1975 – 1977


Mhe. Sailus Mayunga – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1977 – 1978

    Mhe. Abdallah Nungu – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1978 – 1981

Mhe. Peter Kafanabo – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1981 – 1986

 Mhe. John Machunda – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1986 – 1987 


Mhe. Meja Jenerali Mwita Marwa – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1987 – 1990    (aliyesimama mbele)

Mhe. Galusi A. Abedi – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1990 – 1993

Mhe. Abubakari Mgumia – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1993 – 1997

          Mhe. Kanali Mstaafu Anatol Tarimo – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 1997 – 2002 

Mhe. Halima Kasungu – Mkuu wa Mkoa kwa mwaka 2002 – 2006 

Mhe. Dk. Parseko V. Kone – Mkuu wa Mkoa kuanzia mwaka 2016.


Mhe. Mhandisi Mathew John Mtigumwe kuanzia Machi mwaka 2016 mpaka Disemba 2016.

Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi  kuanzia Disemba 2016 mpaka Mei 2021.


                                                                               

Mhe. Dkt. Binilith Saatano Mahenge kuanzia Mei 2021 mpaka sasa.



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Tutapima udongo kabla ya kusambaza mbegu za alizeti RC Mahenge

    June 28, 2022
  • RAS Mwaluko azindua wiki ya utumishi wa umma ki Mkoa, ahimiza viongozi kutimiza wajibu wao na kutoa huduma stahiki kwa mujibu wa sheria katika kuwahudumia Wananchi.

    June 17, 2022
  • "Singida ni Mji Pekee hapa Nchini kuwa na Maziwa mawili" RC Singida

    June 17, 2022
  • RC Mahenge Atatua Kero za Wananchi wa Wilaya ya Itigi.

    June 17, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.