• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Elimu

  • TAARIFA YA MAENDELEO YA KITAALUMA MKOA WA SINGIDA
  •  KWA MWAKA 2021
  • Utangulizi
  • Mkoa wa Singida una jumla ya Shule za Msingi 624; kati ya hizo,  Shule za Serikali ni 587 na za Binafsi 37. Aidha, kuna Shule za Sekondari 167 zikujumuisha Shule 143 za Serikali na Shule 24 za Binafsi. Vilevile Mkoa una Taasisi 10 za elimu ya juu kati yake 1 zipo chini ya Kamisheni ya Vyuo Vikuu (TCU); 8 zipo chini ya Mamlaka ya Elimu na Ufundi (NACTE); na 1 ipo chini ya Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA).

Maendeleo ya Elimu katika Mkoa wa Singida yamekuwa yakiimarika mwaka hadi mwaka. Maendeleo haya ni pamoja na kuboreshwa kwa miundombinu shuleni; kuanzishwa kwa Shule za Binafsi na za Serikali na pamoja na kuongezeka kwa asilimia za ufaulu katika Mitihani ya Taifa.

  • Hali ya Udahili wa Wanafunzi :
  •       Idadi ya Wanafunzi kwa Shule za Msingi 2022
  • Mkoa una jumla ya wanafunzi 434,925 kati ya hao wavulana ni 217,132 na wasichana ni 217,793 ambao wameandikishwa katika Shule zote ndani ya Mkoa.
  • Hali ya utoaji wa Taaluma:
  • Mkoa wa Singida kitaaluma umeendelea kuimarika siku hadi siku jambo linaloonesha maendeleo ya kielimu ndani ya Mkoa. Hii inajidhihirisha kwa kuangalia matokeo ya mwaka 2021.
  •  
  • 3.1.1 Matokeo ya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) mwaka 2021
  •         Mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi (PSLE) mwaka 2021 ulifanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 08 - 09/09/2021.  Masomo yaliyotahiniwa yalikuwa sita (6) ambayo ni Kiswahili, English Language, Maarifa ya Jamii, Hisabati, Sayansi na Uraia na Maadili.  Mkoa wa Singida ulikuwa na jumla ya shule 547 zilizofanya Mtihani huu ambapo Shule za Serikali zilikuwa 530  na binafsi 17.
  •  
  • Idadi ya wanafunzi waliofaulu kwenye Mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2021
  • Jumla wa wanafunzi 28,072 wakiwemo wavulana 15,053 na wasichana 15,019 wamefaulu Mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2021 kati ya wanafunzi 35,773 waliofanya Mtihani. Mwaka 2020 idadi ya wanafunzi waliofaulu ilikuwa 23,785 hivyo kuwa na ongezeko la wanafunzi waliofaulu 1,288 kwa kulinganisha mwaka 2021 na 2020.
  • Asilimia ya Ufaulu ngazi ya Mkoa
  •   Matokeo yanaonesha asilimia ya ufaulu wa Mkoa umepanda kutoka asilimia 71.79 ya mwaka 2020 hadi asilimia 78.9 ambapo ufaulu huu umepanda kwa asilimia 7.11
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2021
  • Jumla wa wanafunzi 12,314 wakiwemo wavulana 5,432 na wasichana 6,880 wamefaulu Mtihani Kidato cha Nne 2021 kati ya wanafunzi 12,314 waliofanya Mtihani. Mwaka 2021 idadi ya wanafunzi waliofaulu ilikuwa 10,748 sawa na asilimia 87.28. Ufaulu huu umeshuka ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2020 ambapo asilimia ya ufaulu ilikuwa 89.20.
  •          
  • Matokeo ya Kidato cha Sita 
  • Mkoa wa Singida ulikuwa na jumla ya shule 15 zilizofanya Mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2021 jumla ya watahiniwa 1,649 walifanya Mtihani ambapo watahiniwa 1,648 walifaulu sawa na asilimia 99.9. Aidha jumla ya watahiniwa 1,564 walifanya Mtihani na 1,462 walifaulu sawa na asilimia 99.8.
  •  

SEKSHENI YA ELIMU

Seksheni hii ina lengo la kusaidia au kuwezesha utoaji huduma za uendelezaji wa Elimu ikijumuisha usimamizi wa elimu ya awali, msingi, sekondari, elimu ya watu wazima na inayotolewa katika njia isiyo rasmi; na mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu. Seksheni hii inaongozwa na Katibu Tawala Msaidizi ambaye pia ni Afisa Elimu wa Mkoa ambaye anawajibika kwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Majukumu ya Seksheni ya Huduma za Elimu
•Kuratibu uongozi wa shule za awali, Msingi, Sekondari, elimu ya watu wazima na Elimu rasmi
•Kuratibu ajira na usambazaji wa walimu wa shule za awali, msingi na sekondari katika Mkoa
•Kuratibu utekelezaji wa sera za Elimu na mafunzo ya ufundi ndani ya Mkoa na kutoa Ushauri kadiri inavyohitajika.
•Kusimamia mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu katika Mkoa.
•Kuratibu ukusanyaji, tathimini, uunganishaji/uandaaji, kutafsiri na kutoa taarifa/takwimu za elimu na mafunzo ya ufundi katika Mkoa
•Kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa taarifa za ukaguzi
•Kuzishauri Mamlaka za Serikali za Mitaa juu ya utekelezaji wa sera ya utamaduni na michezo
•Kuratibu shughuli zinazohusiana na michezo katika Mkoa na kuendesha mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA Mkoani.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru Watua Singida Mjini watoa Siku tatu kwa Tanesco kuhakikisha Umeme umefika shule ya msingi Mwembe Mmoja.

    August 12, 2022
  • RC Serukamba amewataka wakulima waliopewa mashamba kwenye Skimu ya umwagiliaji Itagata kuyaendeleza haraka mashamba hayo.

    August 11, 2022
  • Wakazi wa Kijiji cha Ughandi B Singida Vijijini wamekabidhiwa rasmi Mradi wa maji wenye ujazo wa Lita Elfu 90

    August 11, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Watua Singida Vijijini

    August 11, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.